Friday 25 March 2016

Vijana: Tuangalie uongozi kwa maono ya kihalisia

Na. Dezidery Kajuna

Vijana tunaweza kuleta mabadiliko, tukiwezeshwa na kupewa nafasi katika nyanja mabali mbali. Pia tunaweza kuleta maendeleo  endapo jamii itatuthamini na kutukabidhi madaraka. Tatizo wengi wetu tumeshindwa kujitambua kuwa -tunaweza na tunavipaji. 


Kuna mitazamo mingi juu ya “ ujana”, “kijana”., Ukiacha tafsri zinazogusa umri(ambazo zinatofautiana baina ya nchi na nchi), zaid kijana anapaswa hasa kuwa na sifa zikiwemo; fikra mpya na uwezo  wa haraka wa kuibua mawazo mapya. Wengine wanaita ujana ni damu change inayochemka!

Kijana pia  upambanaji wake ni wa kiujana zaidi.  Haijalishi ni mapambano ya aina gani. Ukumbuke kuna mapambano ya kimaisha yaani mtu binafsi, kisiasa, kijamii, kwa ujumla kupambana kwa ajili ya jamii inayokuzunguka.
Neno uongozi si neno jipya na wala si geni masikioni hata machoni petu ni kimaanisha tunawajua viongozi na tunaweza kuwaona na kuwagawa katika makundi kutokana na uongozi wao na mafanikio yao.  Ila tukumbuke uongozi upo katika makundi ya kwamba kuna ule uongozi wa kimabavu au kiimla na ule uongozi usio kuwa wa kimabavu, unaofuata sheria na katiba zilizowekwa kwa makubaliano katika kikundi, jamii au nchi fulani. 

Kuna kitabu kinaitwa “Uongozi bora” kilichoandikwa na Mahnaz Afkhami,Ann Eisenberg na Haleh Vaziri kwa msaada  wa Suheir AzzouniAyesha Imam, Amina Lemrini, RabĂ©a Naciri -wanasema  Uongozi ni uwezo wa kubuni na kuyaweka maono katika vitendo”.   Japo  kuna vitabu vingi vilivyo andika juu tafsri ya  neno uongozi . Hivyo basi  suala la uongozi ni muhimu kwa kila mtu.

Kwa mtazamo huu haijalishi wewe ni mzee kwa maana ya kwamba  una zaidi ya miaka 40  au upo chini ya miaka 18. Kama wewe ni mzee basi kumbuka unahusika maana wewe ni tunu na ni muhimu katika kumjenga kijana ili awe bora katika siku za usoni. Kama wewe upo chini ya miaka 18 basi kumbuka una fursa ya kujifunza na kujiandaa kuwa kiongozi bora siku za usoni.

Tanzania ni nchi moja wapo iliyobarikiwa kuwa na watu, si maanishi kuwa nchi ikiwa na watu wachache imelaaniwa- , la hasha! Hapana, dhana yangu inabebwa na imani kuwa mkiwa wengi ni rahisi kulifanya jambo gumu kuwa jepesi kwa dhana ya kusaidiana, ujuzi kuwa mwingi kwa idadi ya watu, uzalishaji kuwa mkubwa maana utendaji-  wa ndani unakuwa mkubwa. 

Jambo muhimu kulielewa ni nani anapaswa kuwa kiongozi na nani hapaswi kuwa kiongozi. Wewe kama ni kijana na unataka au unahisi una talanta ya uongozi basi huna budi kuanza kujifunza juu ya uongozi. Kuna njia au nafasi nyingi za kuweza kujiandaa kuwa kiongozi, unaweza shiriki katika mafunzo ya uongozi, warsha za uongozi, mikutano na makongamano yanayo husu uongozi au kujituma pale unapopewa majukumu ya kawaida. 

Mfano unaweza  kuchukua nafasi ya uongozi nyumbani kwa kuhakikisha watu wanafanya kazi kwa misingi ya kugawana kazi, mtaani au kijijini  kwenu unaweza pia kushiriki kutoa mawazo ambayo unadhani yatasadia kuleta amani, uwajibikaji, utendaji madhubuti,  kwa mfano ulipaji wa pesa za taka, usafishaji wa mitaa au vijiji, lakini pia unaweza chukua jukumu la kuongoza watoto hapo mtaani au kijijini, kwa mfano juu ya tabia njema, kuheshimu wazazi, kuwa na upendo katika jamii husika, kusoma kwa bidii, na wao watatambua na kukumbuka kwa mchango wako na hapo ndipo utakapo jifunza ni maana ya uongozi.

Uongozi ni kukubali majukumu na kuyasimamia kwa umakini, utashi, ukarimu, usitaarabu au busara, uwajibikaji, ukweli na uwazi, usawa bila kujali itikadi za kidini, kirangi, kabila au ukanda. Si rahisi sana kuwa na vitu hivi vyote inahitaji moyo, kujituma na kujifunza kutoka kwa watu walio kutangulia, watu unao ongoza na jamii husika inayokuzunguka.

Ikumbukwe kuwa pia kiongozi ni mtu anayeheshimu wa watu wa rika zote bila kujali kiwango cha uelewa wao, umri, elimu yao, na kiasi cha mali walizo nazo. Kiongozi ujifunza kila sekunde,dakika, saa, siku,-wiki, mwezi na hatimaye mwaka. Namaanisha kiongozi ni yule ajifanyaye mjinga kiasi cha kutaka kujua jambo kila siku iendayo kwa Mwenyezi Mungu.

Kama unataka kuwa kiongozi ila una ugonjwa wa kutopenda kuerekebishwa au kuwajibishwa basi jifunze kujishusha. Kujishusha ni siraha kubwa sana kwa mtu anayehitaji kuwa kiongozi bora katika jamii. ‘
Kijana kiongozi, ni mtu anayetegemewa kuwa hana makuu, si mpenda ugomvi, si mlevi kupindukia kiasi cha kuleta kizaazaa kwa jamii husika, si mtu mwenye kashfa maana vijana wengine na hata watu wazima watajifunza mema na mabaya kutoka kwako. Hivyo kiongozi kijana ni yule atakaye epuka haya yote. 

Kwa sasa Tanzania, ni moja ya nchi chache duniani ambazo vijana wake wana hari kubwa katika masuala ya uongozi haswa kisiasa. Ila safari bado ni ndefu maana, uwajibikaji, uwazi na na utendaji madhubuti ni tatizo kubwa kwa jamii nzima, na kwa serikali kiujumla. 

Vijana wa sasa, hapa Tanzania hatuna darasa la uongozi mathalani -serikalini, kwani  serikalini hatujaona mtu wa kuiga au mfano bora katika uongozi, ni majungu, ukabila, ukanda, undugu, rushwa, na ushirikina. -Naomba nieleweke vizuri hapa majungu na-maanisiha watu wamekaa kusemana, kupigana vita na hata kuchongeana maneno yasiyo na tija, ukabila hilo linajulikana sana kwa jinsi viongozi na makabila yao wanavyojineemesha kwa kupeana nafasi za uongozi.  

Undugu, hili si geni, tunajua jinsi ambavyo watu walivyojazana katika maofisi kwa mgao wa kikabila, mtu anapewa kazi au uongozi kwa misingi ya ukabila Rushwa, hii imekuwa kama wimbo, mtu yupo radhi kuitoa roho ya mwenzake kisa amekataa kupokea rushwa, tena rushwa imekwenda mbali zaidi imeingia mpaka katika taasisi nyeti kama mahakama, polisi na hosipitalini na makanisani je ni nani atapona kwa hili? 

 Ushirikina, kwa hili naomba tuelewe kuwa mchawi ni mchawi na mshirikina ni mshirikina haimaniishi unatoka wapi na kabila gani. Ushirikina kwa sasa unatumika kama chombo cha kujikomboa katika uongozi, zamani watu walikuwa wanaomba ruhusa za kwenda kusoma ili kujiongezea elimu kwa maana ya ujuzi ila kwa sasa watu wanaomba ruhusa za kwenda kwa waganga mwishowe taifa linaangamia kwa sababu watu wamekosa maarifa.

Vijana, nawaomba tujifunze kutoka katika hayo niliyoyaeleza, tukumbuke kiongozi hafufuki au haji kwa njia za undugu, ukabila, ukanda au ushirikina. Kiongozi anaandaliwa na kwa kutambua wito uliondani yake mwenyewe. Kiongozi anajifunza kutoka kwa wengine, kiongozi anaenda darasani kusomea ujuzi.

Na uongozi ni wito, si eti kwa sababu baba ni waziri au mbunge basin a wewe unaweza kuwa kiongozi la hasha, kama ni wito utakuwa kiongozi. Ila cha msingi uongozi ni mafunzo ndo maana wenzetu wa nchi zilizoendelea wanaamini mtu aliye na ujuzi na aliyeusomea na kuishi kwa muda ndie kiongozi bora. Vijana amkeni, wakati ndo huu, fursa ni yenu kujifunza, kujitoa kwa ajili ya nchi yetu, kupambana na ujinga, rushwa, ushirikina, kuwajibika kwa uhakika, kuwa wazi, kuwa watendaji wa kweli na kujifunza kutoka kwa walio na mafanikio katika uongozi.

Kiongozi bora hategemei ushabiki wa vyama,  ila anajifunza na kutenda kadri ya sheria za nchi. Kijana aliye na nafasi kuwa kiongozi ni Yule anayetambua kuwa hakuna binadamu aliye juu ya sheria, hakuna aliyekamilika kimaadili, kimawazo, kiutendaji na hivyo kila mtu ana mapungufu.  Tuchague kilicho bora kwa kwa misingi ya kuleta maandeleo. Kama ni kuchagua basi wewe kijana chagua mtu aliye na sifa nilizo zilizotajwa hapo juu, usichague mtu kwa sababu ni mhaya, msukuma, mchaga, mpare, au eti ni kabila lako, hapana usifanye hivyo! 

Pia tusichague mtu eti kisa ana pesa au umepokea pesa kutoka kwakwe. Jifunze kusema hapana kwa ufedhuli wa namna hiyo, jifunze kuchagua kilicho bora, jifunze kuipenda nchi yako na watu wako.
Jambo muhimu la kukumbuka ni kwamba kiongozi bora na kijana mdadisi ni yule asiye penda sifa au kusifiwa vijana wa kileo wanawaita -”mpenda masifa”- na ambaye atakuwa tayari kukosolewa na kujierekebisha. Kiongozi ni yule mwenye siko pana namaannisha aliyetayari kusikiliza watu na mahitaji yao. 

Nakumbuka kuwa niliwahi kugundua kuwa hata wanaoongozwa wanaweza kuwa sehemu ya darasa kwa viongozi. Wale wanaoongozwa si bubu na wala si wajinga ni watu wenye akili timamu na chanya na wana michago mingi sana juu ya kipi kifanyike na kipi kisifanyike. Tujifunze kusikiliza watu tunaoongoza katika nyanja mbali mbali.  Kuna mifano mingi ambayo tunaweza kujifunzia kutoka kwa watu mashuhuri  waliowahi kuwepo na waliopo hapa duniani kwa sasa. ­

Lakini kihisitoria tunajifunza na kupata kujua kuwa Mwana falsafa maharufu  kama Plato katika maandishi yake aliwahi  kusema “ Leaders must understand that their daily choices, judgment calls, behaviors and actions matter and make a difference–they have meaning. Leaders are called to the higher realm of intelligence and accountability and must help others, (akimaanisha kuwa ,  Viongozi lazima waelewe ya kuwa maamuzi, tabia na matendo yao ya kila siku ni muhimu na yana maana. Viongozi wamepewa uwezo mkubwa wa kiakili na kiuwajibikaji na inawapasa kusaidia wengine)

Ni kama vile kauli ambayo akipata kuitoa Mwenyekiti wa Chadema Taifa Mheshimiwa Freeman Mbow akisema kuwa viongozi wanatengenezwa. Ni kweli! Lakini pia  hata taifa madhubuti na lenye mafanikio utengenezwa pia tukirudi kwa Plato aliwahi kusema                  -” therefore we need not to expect to have better states until we have better men”  (akimaanisha,-hivyo basi hatuitaji ku-tegemea kuwa na taifa bora mpaka tupate watu bora-akimaanisha viongozi bora).
Huo ndio kweli, kuwa taifa halijengwi na vijana au watu legelege, wala rushwa, watu wa kuchaguana kiukanda au kikabila bali taifa hujengwa na watu bora yaani viongozi bora. Tuache kulalamika, tukae chini na kasha tutafakari ni kwa jinsi gani tutaweza kujenga viongozi bora kwa sasa na baadae. Wahenga walipata kunena “Usione vyaelea vimeundwa”


No comments:

Post a Comment