Friday 25 March 2016

"VIFO VINGINE SI MPANGO WA MUNGU BALI NI UZEMBE WA MWANADAMU"

Na Dezidery .K

Nalazimika kuandika makala hii ili kuhamasisha mabadiliko katika sekta ya afya. Kwanza kabla ya yote ifahamike kuwa mabadiliko yoyote yale na popote pale si jukumu la serikali peke yake bali ni jukumu la wananchi  katika jamii yoyote inayotaka maendeleo ya kweli.

Tanzania ni mmoja ya nchi masikini zinazo endelea kushuhudia matukio ya kusikitisha sana katika utoaji wa huduma za afya. Utoaji huu wa huduma za afya kwa asilimia kubwa ni ule usiofuata taratibu na kanuni za utabibu. Inawezekana tumepoteza ndugu  wengi kwa uzembe wa manesi na madaktari wasio zingatia taaluma zao. 

Katika hili jamii imekuwa ni- ya kubeba, kuzika na kuombeleza vifo vya ndugu zetu bila kuhoji walakini wa huduma walizo pewa ndugu zetu. Inawezekana ni uelewa mdogo wa watu katika kuhoji haki zao na pia inawezekana ni umakini mdogo wa wataalamu wa afya katika vituo vya afya. 
Ni ukweli usipingika kuwa hakuna anaye penda kufa lakini kwa kuwa kifo ni sehemu ya maisha ya mwanadamu basi siku ikifika hatutakuwa na namna. Lakini si vifo vyote ufuata mpango huo wa maisha ya mwanadamu. Vifo vingine ni matokeo ya uzembe wa aidha upande wa mwadhirika au mtoaji huduma. Hata hivyo tumekuwa tunasingizia Mungu sana, yaani kila msiba ni mpango wa Mungu.

Misiba hii imekuwa ikinakishiwa na maneno kama vile "Ni Mpango wa Mungu". Lakini swali ni Je ni nani mwenye udhibitisho kuwa kifo au vifo hivyo vilikuwa ni matoke ya mpango wa Mungu? Ni swali gumu lisilo na jibu maana lazima jamii ikubali kuwa kuna uzembe mkubwa unfanyika katika vituo vya afya zetu.

Kuna matukio mengi yaliyotokea ambayo ni ishara kuwa kuna uwalakini katika huduma  za afya zinzotolewa katika hosipitali zetu. Moja ya tukio ninalolijua vizuri na pengine kunihuzunisha sana ni kifo cha ndugu yangu. Tukio lilitokea mwaka 2010 mwezi tatu (Machi), ndugu yangu huyu alikuwa amepatwa na homa ya gafra na  baada ya masaa machache alipata msaada wa rafiki zake kumpeleka hospitali ya wilaya ya Temeke (Temeke Hospital), alipofikishwa pale aliwekewa drip, yaani mara nyingi "drip" ndo inakuwaga ya kwanza kabla ya vipimo. Basi, kaka yangu huyu alilala hapo mpaka asubuhi nilipofika hapo akiwa bado na kopo la drip. 

Nilipofika pale nilienda moja kwa moja mpaka kwenye chumba cha manesi, niliulizia habari ya ndugu yangu. Jibu lilikuwa na la mshangao sana, niliambiwa huyu bwana kaja kaletwa hapa akiwa na homa sana na tulipo mcheki tukagundua hana pesa mfukoni hivyo tuka msadia drip. Sasa jiulize drip hiyo mmoja ili msaidia nini katika usiku wote ule pasipo vipimo?

Niliondoka katika chumba hicho cha manenisi kwa mshangao wa majibu yao. Moja kwa moja nilienda katika kitanda cha mgonjwa wangu, kutoka na hali mbaya niliyo ikuta pale ilitubidi tumbadilishe mavazi yake kisha tumtafute daktari, katika haraka hizo ndugu yetu alitutoka na ukawa ndo mwisho wake wa maisha hapa duniani. 

Ni miaka zaidi ya mitano imepita sasa bado najiuliza Je angepata huduma nzuri kwa muda ule wa jioni alipofikishwa pale si angekuwa hai? Au majibu ya vipimo yangetoa mwangaza wa wapi apelekwa ili apate huduma bora. 

Ngoja niishie hapo, hivi majuzi juzi tukio lingine limetokea huko Bunda. Katibu msadizi wa CCM amepoteza maisha kwa staili ile ile. Najiuliza hivi hawa manesi wameajiliwa na nani? Au ni mfumo mzima wa afya umekosa muongozo.  Hayo ni baadhi ya matukio machache tu, lakini tukiomba kufanya utafiti na kuzunguka nchi nzima bila shaka tunaweza pata matukio zaidi ya elfumoja ya namna hii.

Tunahitaji mabadiliko makubwa sana katika huduma hizi. Katika jambo lisilohitaji matabaka ni hili la huduma za afya. Kila mtu ana haki ya kupata huduma za afya bila kujali kipato chake. Nchi inapoteza nguvu kazi kwa uzembe wenye tiba. Serikali inabidi ichambue matatizo kiundani zaidi badala ya kuyaangali kijujuuu tu.

Mabadiliko ni safari na tena yenye mwisho. Mwisho wenyewe ni ufanisi wa utendaji katika mfumo mzima. Palipo na lengo la kweli matokeo uonekana dhahiri.

Hivyo hivyo, sekta ya afya inahitaji mabadiliko makubwa na tena yenye tija bila kujali hudama hiyo inatolewa kwa mtu wa aina gani. Mabadiliko haya yanahitaji malengo ya kweli kwa faida ya wananchi wote.

Mageuzi yasipo fanyika sote tutakuwa wahanga wa "Mpango wa Mungu"

No comments:

Post a Comment