Friday 25 March 2016

MAPINDUZI YA NCHI ZA KIARABU NA UGUMU WA MAISHA BARANI ULAYA

Na. Dezidery Kajuna

Ni mwaka sasa toka mapinduzi katika nchi za kiarabu yaanze. Ukweli ni kwamba dunia imeona mengi hasa mwaka uliopita yaani 2011. Mapinduzi hayo yalileta mkanganyiko kwa wengi hasa watalawa katika nchi nyingi barani Afrika na nchi nyingine za kiarabu. 


Tukumbuke, mapinduzi yale yalianzia Tunisia kisha, Misri  na baada ya siku kadhaa Libya nao wakaanza mikakati ya mapinduzi yaliyopelekea kiongozi wa muda mrefu katika taifa hilo Muammar Ghaddafi kuuwawa.  Wingu hilo la mapinduzi halikuishia hapo bali liliendelea katika nchi nyingine kama vile Yemen, Bahrain na kwa sasa Syria ambako vyombo vya kimataifa vinaharifu kuwa hali inazidi kuwa tete, mamia ya watu wakiangamizana. 

Mada yangu leo si kuzungumzia  juu ya mapinduzi hayo  bali ni kueleza adhari ambazo zimejitokeza haswa kwa upande wa nchi za ulaya ambazo kwa njia moja au nyingine ndizo zilizo chochea moto katika mataifa haya ninayozungumzia. Tulishududia mataifa makubwa kama ufaransa, Marekani,  na washirika wao wakipiga kelele na kulaani utawala uliokuwa karibu na mataifa ninayo yataja kiurafiki katika Nyanja zote kisiasa, kiuchumi na kisiasa. 

 Tukumbuke pia ubabe na uwezo wa vyombo vya kivita jinsi vilivyotumika kuangamiza mamia ya watu kwa misingi ya kutetea demokrasia.  Nina sema kuangamiza watu kwa sababu naamini kuwa demokrasia si kuangamiza watu bali ni mazungumzo na maelewano kati ya pande zinazo zozana.

Ukweli utabaki kuwa pale pale kuwa mwaka 2011 haukuwa mwaka mwepesi au raisi kwa mataifa mbali mbali. Japokuwa tuna la kujifunza kama watanzania. Na kumbuka kipindi cha vuguvugu hili la mapinduzi huko Afrika kasikazini vuguvugu hilo lilinukia pia hapa Tanzania. Chadema hawakuwa nyuma, nao walikuwa na lao katika kupambana na utawala wa Mheshimiwa Jakaya Kikwete.  Naomba nieleweke hapa, Chadema walikuwa si  tu wanapambana , bali walikuwa wanatetea na kupigania haki za watanzania kuwa na maisha bora, katiba bora, kulikabili anguko la uchumi. Nguvu za dola zilitumika sana japo hazikushinda nguvu ya umma.

Uganda pia nako kulikuwa na vuguvugu la aina yake , naweza kulifananisha vuguvugu lile na hili la Tanzania.  Japo kule nchini Uganda Dk. Kizza Besigye na washirika wenzake hawakufanikiwa sana kama hapa Tanzania hii inatokana na aina mfumo na mtandao wa  wanachadema kuwa imara sana na  kulinganisha na majirani zetu Uganda. Sitaki kulizungumuzia hili ila kiufupi ni kwamba utawala wa Uganda ni wa kijeshi, kiundugu mpaka hata kwenye taasisi nyeti kabisa na Rais hawezi kusalitiwa kwa maana hana mtandao bali anaabudiwa na wote walio nae katika utawala wake kama sehemu ya fadhira. 

Nirudi kwenye mada yangu, vuguvugu lile la mapinduzi limeleta baraa kubwa katika barani Ulaya katika nchi nyingi haswa Ulaya mashariki na baadhi ya nchi ya ulaya magharibi. Adhari hizi zinatokana na sera, mahusiano yaliyopo na nchi husika zilipo kwenye machafuko, pia na nafasi ya nchi katika baraza la umoja wa mataifa katika kusaidia wakimbizi. Na ikumbukwe pia machafuko haya yaliambatana  na anguko la KIuchumi duniani mbalo bado lina sumbua sana nchi nyingi duniani. 

Kule nchini Italia hali ilikuwa mbaya sana mbali na uchumi wa nchi hiyo kuwa mmbaya wakimbizi walikuwa wengi sana wengi wao wakitumia njia ya bahari kwa kutumia vyombo hatarishi. Italia ndio nchi pekee inayosemekana kuwa ilipokea wakimbizi wengi kutoka Libya. Ifahamike kuwa nchi za ulaya huwatambua wakimbizi kama raia wao, na pia upewa haki sawa kama raia wengine. Ongezeko hili la watu, limepelekea kuwepo tatizo kubwa la ajira kwa raia walio wengi haswa vijana. Maandamano yalikuwepo kila wakati na mwisho wa yote ili lazimika Waziri Mkuu Silvio Berluscon  kujiuzuru huku rais wan chi hiyo Giorgio Napolitano akimteua Mario Monti kuwa Waziri Mkuu mpya sambamba na kukabiliana na hali ya kichumi. 

Hali hii iliikumba pia nchi ya Ugiriki, watu wengi wanadhani hali ya kiuchumi tu ndio imepelekea mataifa haya makubwa kukumbwa na misukosuko, la hasha! Ugiriki ni nchi moja wapo isiyokuwa na sera na mikakati madhubuti ya kupambana na ongezeko la wahamiaji. Na hili lilipelekea uchumi wa nchi hiyo kudorora mpaka kupelekea waziri mkuu wan chi hiyo  George Papandreou  kujiuzuru. Huku waziri mpya Lucas Papademos akiteuliwa lakini hali bado si nzuri.   

 Nchini Ufaransa Taifa kubwa kabisa lakini nalo nadhani linajutia sana maamuzi yake ya kuingilia mambo ya Kisiasa kwani inaelezwa kuwa nayo ni nchi mmoja wapo iliyopokea wahamiaji wengi, wengi wao wakitoka Tunisia, Ivory coast na pia Libya. Ajira ni tatizo kubwa nchini Ufaransa kwani, kila kukicha kuna ongezeko kubwa la wahamiaji na wengi wao hawana makazi na ajira ukilinganisha nchi zingine kama Uingereza, Ujerumani, Sweden, Norway, Uholanzi, na Finland.  Wizi kama ule wa kariakoo wa kukwapua mabegi ya watu au simu unaripotiwa kuwa ni kama jambo la kawadia kwa sasa nchini Ufaransa. 

Nchini Sweden, Norway na Finland madhara  ya wimbi la mabadiriko ya kisiasa Afrika magharibi na mashariki ya kati zinaonekana haswa katika Nyanja ya ajira na si makazi. Ajira nyingi haswa kwa wageni  wanao zamia na wanaoenda kwa ajili ya masomo imekuwa tabu sana. Hii inatokana na sera ya nchi hizi kuwathamini sana wakimbizi hasa wale waliopokelewa na mamlaka husika kwa kuzingatia vigezo vya shirika la kusaidia wakimbizi duniani. 

 Nchini Sweden, serikali inahusika moja kwa moja kuwatafutia kazi wakimbizi, kuwapatia makazi, na pesa ya kujikimu  kupitia almashauri za nchi hiyo.  Hivyo imepelekea pia raia wengi kutoka barani Afrika na sehemu zingine kukosa ajira hasa walio masomoni na wahamiaji haramu (wasio tambuliwa).  Naomba ifahamike kuwa mkimbizi anayetoka katika nchi iliyo kwenye machafuko anathaminiwa sana na kulindwa kuliko yule aliyetoka nchi zisizo kwenye machafuko  kama Tanzania, Kenya, Uganda na nchi nyingine nyingi. 

Ongezeko hili la watu limekuwa ni bomu jipya katika nchi hizi za ulaya, na hii imepelekea kuanzishwa kwa mchakato wa kupunguza idadi ya wakimbizi, kutopokea wakimbizi kwa maana ya kuwasaidia ndani ya mipaka ya nchi zao. Lakini pia hatua zaidi zimechukuliwa ikiwa ni pamoja na kulinda mipaka ya nchi, kwa kuanzisha  mfumo jumuishi  wa mkutambua mtu kwa kutumia vidole vya mhusika balani ulaya kote .

 Nacho maanisha hapa ni kwamba kwa sasa kila raia awe ni mzaliwa wa hapo au muhamiaji wote watakuwa na vitambulisho vilivyo na alama za vidole vyao zilizochukuliwa kwa mashine maalumu. Kwa hiyo kuvuka mipika ya nchi mmoja kwenda nchi nyingine itakuwa kazi kweli kweli.  Mfano mzuri ni Sweden ambao wao wamekwisha anzisha mifumo yote hiyo pamoja na punguzo la  kupokea wakimbizi kwa asimilia tisini na nane kuanzia mwaka jana. 

Kwetu hapa Tanzani sidhani kama mambo haya yanawezekana kwa maana hatuna mifumo dhabiti ya kukabiliana na wakimbizi, utawala haupo makini, rushwa inatumika sana na uelewa wa waliopewa mamlaka ni mdogo sana. 

Tunahitaji mapadiliko makubwa katika chombo chenye dhamana husika. HIli nalo ni bomu ambalo linaweza kuongeza adhari zaidi kwetu kwa maana ya kwamba tayari tumekwisha shuduhudia adhari hizo ikiwa ni pamoja na waasia tunao waona hapa nchini ambao wengi wao wameingia kinyemera kwa msaada wa rushwa. Ajira nyingi ndani ya viwanda vinavyo milikiwa na wahindi , wapakistani na wachina zimechukuliwa na wageni huku wenyeji wakiwa hawana pa kukimbilia. Tunahitaji mabadiliko katika jambo hili, na hatua muhimu lazima zichukuliwe. Tunahitaji kusimamia raslimali zetu vizuri, mazingira bora ya kazi kwa watanzania  ni haki yetu na ni wajibu wa serikali kuwa sera mbadala na mikakati madhubuti katika kulisimamia jambo hili.

No comments:

Post a Comment