Friday 8 January 2016

KALAMU KUTOKA TANZANIA

OCTOBER 06, 2013
Kwanza kabisa natoa pole kwa wale wote waliousurika  na janga la kuzama kwa boti baharini nchini Italia katika kisiwa kiitwacho "Lampedusa",  wengi wao wakitoka pembezoni kasikazini mwa Afrika kuelekea barani Ulaya. Na Mungu azilaze roho za marehemu waliofia baharini mahari pema peponi. 


Baada ya tukio la kuzama kwa meli nilijihisi mtu mwenye maumivu mengi moyoni na huzuni ikinitawala juu ya vifo vya vijana wenzangu wa Afrika- tukubali kuwa tumepoteza nguvu kazi ya Afrika!


 Licha yatukio hilo  kuniudhunisha, limenikumbusha matukio ya aina hiyo kuwahi kutokea hapaTanzania.  Suala la uhamiaji ni changamoto kubwa  si ulaya tu kama vyomba vya habari vya magharibi vinavyo taarifu bali ni duniani  kote, bara la  Afrikal likiwa la kwanza hususani hapa Tanzania. 

Tanzania kiujumla kuna wahamiaji wengi mithili ya walioko huko nchi za Magharibi  japo tofauti ni  ya kijiografia.  Lakini Je ni kwanini matukio haya kutokea?

Waafrika tumeaminishwa kuwa Ulaya ni mahali pazuri pakuishi na kazi hupatika kiurahisi  na hii ndio sababu ya kubwa ya wimbi la  wahamihaji  kuongezeka kila kukicha. Matatizo ya kiuchumi yanayo sababishwa na kuchangiwa miundo mibovu ya uduma za kijamii na serikali dhaifu za Afrika ndio sababu nyingine inayotajwa kushindwa kutengeza au kuzalisha ajira kwa watu wake hususani vijana na mwishowe kukimbia nchi. 

Tanzania imekuwa ikishutumiwa sana kuwa ni "njia" au "uchochoro"  wa kupitisha wahamiaji haramu hasa wanaotoka chini Eritria, Somalia na Ethiopia kwenda barani Ulaya. Tukio la Lampedusa ni ishira ya jinsi gani matukio au suala la uhamiji linavyoanza kuwa ni "majanga".
Hapa nchini Tanzania, Mikoa ya Tanga  Arusha, Morogoro, Iringa, mbeya ndio njia maarufu kwa wasafiri hawa haramu. Pengine ni kwa sababu ya mfumo mbovu wa serikali yetu wa kulinda mipaka yake na haswa suala la rushwa miongoni mwa baadhi ya maafisa wa uhamiaji.

Lakini, cha kusikitisha zaidi ni kuwa tukio la kuzama kwa meli huko "Lampedusa" halina tofauti na matukio ya vifo vya wahamiaji wapitiao nchini Tanzania kuelekea nchini Afrika ya kusini kisha barani Ulaya.  Lakini Je, wahamiaji hawa husafirishwa kivipi kupitia Tanzania? 

Taarifa mbalimbali kutoka katika vyombo vya habari hapa Tanzania, vinasema wahamiaji hawa haramu husafirishwa kwa  siri kama biashara zozote zile za magendo. Taarifa hizo uonyesha kuwa  makontena makubwa yaliyozibwa na kuachwa sehemu ndogo ya  hewa , magari ya mizigo yaendayo nchi za jirani na magari madogo hutumika kusafirishia watu hawa huku wahamiaji hao wakitoa pesa kwa ajili ya usafiri huo.

Kwa mujibu wa nakala ya gazeti la Tanzania Daima la nchini Tanzania la  tarehe 28,juni mwaka jana ukurasa wa Tahariri Mwahariri anasema, nanukuu ‘’ Siri ya vifo vya raia wa Ethiopia 42 waliofariki dunia kwa kukosa hewa kwenye roli la mizigo kwenda nchini Malawi, imejulikana. Habari ambazo gazeti hili limezipata kutoka kwa majeruhi wa tukio hilo, zilisema kuwa walipoteza maisha kutokana na kukosa chakula baada ya kukaa kwenye roli kwa miezi mitatu mfululizo.
Mmoja wa majeruhi 72 walionusurika, aliliambia gazeti hili kuwa tangu walipoanza hadi siku waliyokutwa kwenye roli wilayani kongwa,Dodoma walikuwa wamemaliza miezi mitatu wameishiwa chakula walichokihifadhi.’’ Mwisho wa kunukuu.

Ikumbukwe pia, Machi mosi, mwaka huu, katika maeneo ya kitumbi Barabara ya Segera-chalinze, kulitokea vifo vya Waethiopia wakiwa ndani ya makontena wakisafilishwa kutokea Arusha kuelekea Dar es salaam. Ambapo baada ya kukamatwa baadhi walikuwa wameisha kufa na wengine wakingali hai hizi ni kwa mujibu wa taarifa ya Mkuu wa mkoa wa Tanga Mh.Constantine Massawe

 Mkuu wa mkoa huo alisema, wahamiaji 54  walikamatwa wakiwa kwenye makontena yaliyokuwa yamewabeba walichanganywa na mizigi ya vitu kama vile  nondo hata hivyo madereva wa magari hayo mawili walitokomea kusikojulikana. 

Lakini swali ninalo jiuliza kwa nini nchi ya Tanzania hakuchuka hatua kama walizo chukuwa maofisa wa serikali ya Italia?... Ndo maana nasema tukio lile la kisiwa cha Lampedusa halina tofauti na Tanzania. Kwa Mujibu wa Waziri wa mambo ya ndani

Swali ni Je matukio ya aina hii yataisha lini? Waafrika tubadilike, Afrika bado ni nzuri na yenye fursa nyingi. Kukimbia matatizo yaliyopo Afrika si sululisho la maisha yetu. Ni lazima tuyakabili kwa kupambana na mifumo duni ya serikali zetu ili yuweze kujenga fursa za ajira.

Lakini pia tatizo hili si la Tanzania na Italia bali ni tatizo la kila nchi hapa duniani. Ufumbuzi unahitaji nguvu ya pamoja ikiwa na pamoja na kujenga mifumo endelevu ya ajira.
"Mwenzio akinyolewa na wewe zako tia maji".

No comments:

Post a Comment