Friday 25 March 2016

"VIFO VINGINE SI MPANGO WA MUNGU BALI NI UZEMBE WA MWANADAMU"

Na Dezidery .K

Nalazimika kuandika makala hii ili kuhamasisha mabadiliko katika sekta ya afya. Kwanza kabla ya yote ifahamike kuwa mabadiliko yoyote yale na popote pale si jukumu la serikali peke yake bali ni jukumu la wananchi  katika jamii yoyote inayotaka maendeleo ya kweli.

"ULAYA HAKUNA MAISHA MAZURI"

Na. Dezidery Kajuna

"Ulaya kuna maisha mazuri" huu ni usemi maarufu sana barani Afrika na nchi nyingi za Amerika ya kusini na Kasikazini. Nakumbuka "enzi" fulani hivi wakati nasoma shule ya msingi, niliwahi kuwa mtu mzuri wa kuadithia watu juu ya jinsi ulaya kulivyo kuzuri. Tena nakumbuka jinsi nilivyokuwa naelezea maisha ya huko utadhani nimezawaliwa huko. Wenzangu wakidhani mimi nimetoka huko majuzi juzi tu, huku walinikodolea macho  mithili ya "watoto" wa uswahilini watazamao filamu ya "Rambo" iliyo tafsiriwa katika lugha ya kiswahili.

INAWEZEKANA

Na. Dezidery Kajuna

Kwa kuelewa kichwa cha mada basi ni matumaini yangu kuwa utakuwa umeweza kujua kinachoelezwa katika mada hii. Hata kama imekuwia vigumu kuelewa kichwa cha ujumbe huu basi utakuwa unafahamu fika ni nini maana ya inawezekana. Bidamu wengi tuna imani katika uwezekano wa jambo fulani kutokea. Nachomaanisha hapa ni juu ya uwezekano wa neno, kitu  au jambo fulani kutokea au kufanyika kwa nguvu za kibinadamu au kimungu. Lengo  langu hapa, si kuelezea kile kinachowezekana “kimungu”, hapana nacho nataka kueleza hapa ni juu ya kile ambacho kwa utashi wa kibinadamu kinawezekana.  

HESHIMA HAINA UMRI!

Na. Dezidery Kajuna.

Ni asubuhi ya saa tano, natoka ndani ya nyumba ninayoishi katika mtaa huu wa Prästgatan hapa nchin Swedeni tayari kwa ajili ya kwenda shule maarufu kwa jina la SFI  (Svenskundervisning för invandrare) kwa lugha ya kiswahili ikiwa na maana ya elimu ya lugha ya kiswidi kwa wahamihaji au wageni. Ni shule mahususi kabisa kwa ajili ya wale wanao penda kujifunza lugha hii ya kiswidi ili iwe rahisi kwao kuwasiliana na wenyeji.

MAPINDUZI YA NCHI ZA KIARABU NA UGUMU WA MAISHA BARANI ULAYA

Na. Dezidery Kajuna

Ni mwaka sasa toka mapinduzi katika nchi za kiarabu yaanze. Ukweli ni kwamba dunia imeona mengi hasa mwaka uliopita yaani 2011. Mapinduzi hayo yalileta mkanganyiko kwa wengi hasa watalawa katika nchi nyingi barani Afrika na nchi nyingine za kiarabu. 

Vijana: Tuangalie uongozi kwa maono ya kihalisia

Na. Dezidery Kajuna

Vijana tunaweza kuleta mabadiliko, tukiwezeshwa na kupewa nafasi katika nyanja mabali mbali. Pia tunaweza kuleta maendeleo  endapo jamii itatuthamini na kutukabidhi madaraka. Tatizo wengi wetu tumeshindwa kujitambua kuwa -tunaweza na tunavipaji. 

Friday 8 January 2016

KALAMU KUTOKA TANZANIA

OCTOBER 06, 2013
Kwanza kabisa natoa pole kwa wale wote waliousurika  na janga la kuzama kwa boti baharini nchini Italia katika kisiwa kiitwacho "Lampedusa",  wengi wao wakitoka pembezoni kasikazini mwa Afrika kuelekea barani Ulaya. Na Mungu azilaze roho za marehemu waliofia baharini mahari pema peponi.